Revealed: Seven Tanzania-tycoons-with-offshore-accounts

By Wikileaks01 Spy

Seven Tanzanians have about $40 million (TSh64 billion) stashed in offshore accounts in British Virgin Islands and Jersey, The Wikileaks01 can reveal today.

 The revelation comes in the wake of reports that the committee set up by the Tanzanian government to trace the owners of the $196.87 million allegedly kept in Swiss banks has failed to come up with adequate evidence.

 According to leaked offshore data obtained by the UK’s Guardian newspaper in collaboration with the International Consortium for Investigative Journalists (ICJ) and analysed by over 110 journalists worldwide, seven Tanzanians operate offshore accounts.

 The ICIJ’s exploration of offshore secrets began when a computer hard drive packed with corporate data arrived in the post. Gerard Ryle, the ICIJ’s director, obtained the small black box as a result of his three-year investigation of Australia’s Firepower scandal, a case involving offshore havens and corporate fraud.

 The hard drive contained more than 260 gigabytes, the equivalent of half a million books. Its files included two million emails and four large databases. There were details of more than 122,000 offshore companies or trusts, and nearly 12,000 intermediaries (agents or “introducers”).

Unlike the smaller cache of US cables and war logs passed in 2010 to WikiLeaks, the offshore data was not structured or clean, but an unsorted collation of internal memos and instructions, official documents, emails, databases and spreadsheets, scanned passports and accounting ledgers.

 The leaked data, also seen by [private daily] The Citizen, could shed light on how the offshore account holders operate to avoid being detected by relevant authorities.

 The Citizen understands that there are legitimate uses for offshore companies and trusts. This being the case, the revelation of Tanzanians operating offshore accounts does not intend to suggest or imply that the individuals have broken the law or obtained their billions illegally.

 According to the leaked data the seven individuals, listed as officers and master clients, all have addresses in Dar es Salaam.

 They are Mr Andre Schmid, Mr Kaniz Mehbub Manji, Mr Mehbub Yusufali Manji, Mr Rameshchandra Chotalal Somani, Mr Stuart Hugh Macdonald and Mr C Rameshchandra Somani.

 It is not clear whether these Tanzanians acted as underlying officers in offshore banking or are the real owners of the billions wired into their accounts in Virgin Islands.

 

By Yericko Nyerere

LEMA: Mh Rais Kikwete, mbona umeamua kuangamiza Taifa?

By
Godbless J Lema

Mh Rais, nakusalimu!

 Kauli yako iliyonukuliwa na vyombo mbambali mbali vya habari wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wako wa NEC (CCM ) ni kauli hatari na yenye laana kubwa sana ya damu za Watu wengi katika Taifa letu. Ninaona wakati mgumu mwingine ambao Taifa letu linaingia kwa sababu ya kauli yako ambayo sasa imetangaza mauaji rasmi yatakayoongozwa na Viongozi mbali mbali wa CCM Nchi nzima huku Polisi wakiendelea kusimamia kama kawaida yao.

 Mh Rais , Kwa mujibu wa maneno yako umethibitishia Umma wa Watanzania kuwa mmejadiliana kwenye kamati Kuu na kukubaliana kuwa sasa yale mambo mliyokuwa mnayafanya kwa kificho sasa yamethibitishwa na Kamati Kuu ya Chama chako na kutangazwa na wewe mwenyewe kuwa , kuumiza , kuua , kutesa na kudhalisha sasa imekuwa sera rasmi ya CCM na umeithibitisha kauli hiyo mbele ya Wajumbe wa Baraza Kuu la CCM ( NEC).

 Mh Rais , kwa kauli hii naomba nikuambie kuwa umeamua kumalizia kipindi chako kwa mikono iliyojaa Damu na Roho za Watu . Nafasi uliyonayo ni kubwa sana sio jambo jepesi kuona makosa makubwa au madogo na kutubu , wapambe ni wengi ambao kwa kumsifu Mfalme hata kwa ujinga maisha yao na ya watoto wao yataendelea kuwa bora , lakini nakuhakikishia kwa kauli hii iko siku utajuta na kulaani ni kwanini ulitoa kauli mbaya na yenye hatia kama hii kwa Kiongozi mkubwa wa Nchi kama wewe . Vijana wa CCM sasa wamejipanga kuua na kuchinja hadharani kama ambavyo umeagiza wafanye na Polisi watakuwa Kimya kabisa kama ambavyo siku zote wamekuwa lakini mara hii watasaidia wazi wazi kabisa unyama wote utakaofanywa kwani wao pia wamesikia Amri yako na wewe ndio Mkuu wa Nchi hii.

 Mh Rais, mambo mengi yanachangia kuvurugika kwa Amani lakini moja kubwa ni pale Polisi na Mahakama zitakaposhindwa kutenda wajibu wake katika kutenda haki haswa pale uonevu unapokuwa dhahiri . Naweza kutambua matendo yote mabaya yanayotokea wakati wa Uchaguzi kuwa yamesababishwa na Upendeleo wa Jeshi la Polisi kwa Wanachama wa CCM pindi wanapofanya uhalifu dhidi ya wenzao wa Vyama Vingine vya Siasa. Mwaka jana 2013 wakati wa uchaguzi wa marudio wa Madiwani wa kata nne Arusha Mjini watu zaidi ya 16 waliumizwa vibaya na Green Guard na matukio yote yaliripotiwa lakini mpaka leo hakuna Mtu aliyefikishwa mahakamani kujibu mashitaka, lakini unakumbuka na unajua kuwa mkutano wetu wa kufunga Kampeni hizo za Udiwani ulipigwa BOMU na Watu Wanne waliuuwa na Zaidi ya 100 kuumizwa vibaya na wengine wamebaki na Vilema hata leo na tumekuomba uunde tume ya Kimahakama ili tukuletee Wauaji wa watesaji wa tukio hilo lakini mpaka leo umegoma na badala yake zimekuwepo jitihada nyingi zinazofanywa na Jeshi la Polisi kubambikia Watu kesi nikiwemo mimi na kutesa watu kwa kiwango ambacho hakielezeki.

 Mh Rais, Watu wameteswa na wanaendelea kuteswa sana katika Nchi hii na kazi hiyo inafanywa na Polisi na ccm na hapa ndipo mashaka katika jamii yanatokea na Jamii kuona ulinzi wao huko mikononi mwao na sio mikononi mwa Polisi na sheria za Nchi. Sasa umetangaza Watu wapigwe na wachinjwe hadharani , jambo ambalo nina uhakika nalo ni kwamba umeamua kuangamiza Nchi uliyoapa kuitetetea na ulioagiza wapigwe sina uhakika kama watakua wamelala chini wakati wanapigwa au wamefumba macho wakati wanateswa na kama itakuwa kinyume maana yake kutatokea Ugomvi ambao madhara yake mimi kwa sasa sielewi ila wewe MKUU uliyotoa amri utakuwa unajua.

 Mh Rais, Wewe wewe ndiye Amiri Jeshi Mkuu umeshindwa kuamrisha Polisi walinde Raia na mali zao na sasa umeamua Watu wachinjane? kwa kauli hii unasubiri nini Ikulu ? Hata hivyo Nguvu ulizonazo sio Imara sana kama Nguvu alizonazo Mwenyezi Mungu . Mateso na Damu iliyomwagika katika Taifa hili kwa uzembe wa utawala wako hakika utalipa kama sio wewe Watoto wako na Wajukuu zako elewa kuwa hakuna dhambi itakayopita bila kulipwa. Kauli yako hii inaleta hofu kubwa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 lakini hatutaogopa kufanya kampeni kwa sababu Rais ameruhusu tupigwe na tuchinjwe, tutasonga mbele kutafuta haki tunayoamini kama ambavyo pamoja na matangazo mengi ya malaria kuua lakini hatujawahi kutembea huku tumevaa chandarua .

 Mh Rais wewe sio Mungu , hata hivyo unamkumbuka Jean Kambanda aliyekuwa Waziri Mkuu wa Rwanda mwaka 1994 alishatakiwa kwa kutoa kauli kama yako na kugawa mapanga kwa Vijana wa Nterahamwe na kusababisha mauaji makubwa sana Rwanda na tarehe 18/7/1997 alikamatwa Nairobi na baadae alishitakiwa na kufungwa Maisha kwenye mahakama ya ICTR Arusha na hii ilikuwa tarehe 4 sept 1998, sikufundishi uoga hata kidogo ila ni muhimu kujadili historia muhimu kulingana na wakati.

 Mh Rais thamani yako haitatokana na kusababisha CCM iwe madarakani tena bali Haki kuwa madarakani katika kipindi ulichotawala ni hekima ngumu kuielewa lakini ni lazima tuiseme. Tunaenda Kalenga kupigwa na kuchinjwa kwa sababu tu umewapa Watu wako ujasiri wa kufanya hivyo lakini elewa kuwa kila tukio litakalosababishwa na kauli zako ni tukio ambalo utalipa gharama zake. Makala zangu kama hizi uwezi kuzipenda sana Mh Rais, Wapambe watakuambia huyu kijana ni muhuni na maneno mengi ya kejeli lakini elewa kwamba anayekupenda ni anayekuambia ukweli, kwani ukweli thamani yake ni kubwa mno hata kama una madhara ya muda.

 Mh Rais, Ninapata hofu ninapoandika waraka huu kwani kama ni kwazo basi unaweza kuamua kufanya chochote dhidi yangu lakini napata faraja kuwa kifo kipo tu hata kama utafuti haki na ukweli kwani Bibi yangu kule Machame hakufa kwa kuwa aliandika waraka bali ni umri tu ulimuondoa. Mh Rais ukweli nakuambia usipofuta kauli yako yenye lengo baya kwa Nchi yetu basi nimemuomba Mungu afanye jambo muhimu dhidi yako na jambo hilo muhimu liko wazi kuwa kama wewe ni chanzo cha Taifa kuharibika kwani nini anaendelea kukupa pumzi? Hapa nitaonekana muhuni tena lakini Mh Rais wema wako ni katika haki na sio sifa.

 Mwisho, Mh Rais, Mamlaka yana tabia ya kudanganya akili nikuombe Rais wangu usikubali mamlaka ikudanganye hata kidogo, futa kauli yako, watakaokuona mjinga wao ndio wajinga. Najua Polisi na Jeshi wanakutii wewe lakini Dhambi na hila iko mbali na MUNGU.

 Godbless Lema (Mb)

By Yericko Nyerere

Vita vya YOM-KIPPUR na funzo kwa dunia

By

  Yericko Nyerere

 

Tupokwenye miaka 40 toka vita vya YOM-KIPPUR kuanza vita hii ilianza tarehe 06-10-1973 nchi za kiarabu zilijipanga vilivyo ili tu kurejesha ardhi zao walizopoteza katika vita vilivyovunja record ya Dunia vita vilivyopiganwa kati ya nchi za Ki-arabu na Israel kwa mda wa siku sita Mwaka 1967 na majeshi ya nchi za Ki-arabu kusalimu Amri na kuacha ardhi zao kutekwa na askari wao kwa mamia kupoteza maisha yao na Maelfu kutekwa.

 Vita hii iliacha maumivu na makovu makubwa sana katika ulimwengu wa Kiarabu hata kupelekea nchi hizo hasa Misri na syria kuanza mikakati ya kukomboa ardhi zao zilizotekwa na Mjeshi ya Israel,kwa maana syria milima ya Ki-mbinu ya Golan ilikuwa imetekwa na kwa upande wa Misri ilipoteza Jangwa lote la sinai ikiwa pamoja na Mfereji wa Suez nchi hizi zilikuwa na machungu sana hasa ikichukuliwa kuwa nchi iliyowashinda ni ndogo sana hivyo mipango iliyofanywa mwaka 1973 ni kuzikomboa ardhi zilizotekwa baadaye kuifutilia mbali Israel katika uso wa Dunia.

 Mipango ya kuivamia Israel ilipangwa ifanyike siku ya Jumamosi ambapo kulikuwa na sikukuu ya Kiyahudi inayojulikana kama YOM-KIPPUR,Siku hiyo Israel ilipata changamoto kubwa ambayo katika historia ya nchi hiyo Kivita haijawahi kutokea, maana siku hiyo Maelfu ya vifaru na Makumi elfu ya Majeshi na ndege za kijeshi zilifanya shambulizi la kushitukiza na kwa pamoja katika mipaka ya Israel ya kusini na kaskazini hii ilikuwa Ishara tosha kuwa Syria na Misri zilikuwa zinataka kurudisha ardhi zao zilizotekwa katika vita vya siku sita vya mwaka 1967.

 CHANZO CHA VITA YA YOM-KIPPUR.  Baada ya Israel kushinda vita vya 1967 Israel ilipata ardhi kubwa ambayo ilipaswa kulindwa kwa gharama yoyote ili kupata Muafaka wa kisiasa kati ya nchi hiyo na nchi za Kiarabu kwa upande wa Misri Israel ilichukua Sinai na Suez canal hivyo Jeshi la Israel lilipata changamoto kubwa sana kulinda mpaka wote wa sinai na Mfereji wa Suez,Majeshi ya Israel yaliweka vituo vya ulinzi vilivyojulikana kama BAR-LEV line,na kwa upande wa Syria Israel ilichukua Milima ya Golan ambayo kwa Israel lilikuwa eneo jipya lililotakiwa kulindwa kwa nguvu zote maana Ki-Jeshi lilikuwa ni strategic la kimbinu sana Maana milima hiyo ya Golan iko kwenye mwinuko kwa hiyo eneo hilo likishikiliwa na Syria ina maana Majeshi ya Syria yana Uwezo wa kumiliki Kijeshi ndani ya Israel kilomita zaidi ya 25 na wakati huohuo Israel haingekuwa na uwezo wa kupata target Shabaha nzuri kupiga majeshi ya Syria yaliyoko kwenye milima hiyo ya Golan na ndiyo maana mpaka leo Israel haiwezi kuiachia milima hiyo maana kufanya hivyo ni sawa na kujitoa MHANGA kwa jeshi la Israel,Badala yake Inataka kuirudisha milima hiyo kwa kubadilisha na AMANI na Syria ili wawekeane mkataba wa AMANI na kutoshambuliana na Israel ili iweze kupata uhakika wa kutoshambuliwa toka milima hiyo ya Golan.

 Baada ya vita vya 1967 Msri na Syria zilianza kujenga majeshi yao ili waweze kukomboa ardhi zao zilizotekwa, Nchi hizo zilihitaji zana za kivita zaa kisasa ili kuweza kummaliza adui yao Israel walihitaji sana kupata silaha toka Urusi wakati huo USSR Walihitaji kupata Ndege aina ya MIG na vifaru aina ya T-62 Vilevile makombora ya kuangushia ndege aina ya SA-2,3,6 na SA-7 pamoja na silaha za kubomolea Vifaru aina ya SAGGER ANT-TANK GUIDED MISSILES.

 Kufikia mwezi October 1972 Rais wa misri wakati huo Anwar Sadat aliwahi kuongea na makamanda wake kuhusu kuishambulia israel na ilipofikia mwezi may 1973 vyombo vya kijasusi vya Israel vilikuwa vimepata habari kuwa Misri itaishambulia Israel kupitia mfereji wa Suez Misri walikuwa wanajua kuwa kama Misri itaishambulia Israel basi Syria nayo ingejiunga na kuishambulia Israel kutokea Kaskazini. Vilevile Israel walidaganyika kuwa Misri itaishambulia Israel mara tu itakapopokea ndege aina ya MIG-23 na SCUD-D toka Urusi Jeshi la Israel lilijua kuwa Misri haijapokea silaha hizo toka Urusi hivyo iliamini Misri haiwezi kuanzisha vita hivyo kabla ya kupokea silaha hizo toka Urusi.

 Mwezi May na Mwezi August 1973 Majeshi ya Misri yalifanya mazoezi makubwa ya kijeshi katika eneo la mpaka na Israel,Israel nayo ilipoona hivyo ilianza kukusanya askari wake kwa maandalizi ya vita lakini baada ya pale hakukuwa na harakati zingine za kijeshi katika eneo hilo la mpaka hivyo Jeshi la Israel liliona kuwa hiyo ilikuwa kawaida tu yaani waliona kama yalikuwa mazoezi ya kawaida tu.

 Septemba 25,1973 Mfalme hussein wakati huo alikutana na waziri mkuu wa Israel wakati huo Mama Gold Meir wakati huo Mfalme Hussein alishakutana na Rais Sadat na Assad wa Syria na alimwonya waziri mkuu wa Israel kuhusiana na kukalia eneo la Syria la milima ya Golan na Sinai eneo la Misri,Baada ya kumalizika kikao hicho na Mfalme Hssein waziri mkuu wa Israel pamoja na waziri wa ulinzi wa Israel wakati huo MOSHE DAYAN pamoja na vyombo vya Kijasusi vya Israel waligundua moja kwa moja kuwa Misri ingewashambulia wakati wowote.

 Masaa machache tu kabla ya Misri kuishambulia Israel tarehe 06-10-1973 waziri mkuu Golda Meir na waziri wa Ulinzi Moshe Dayan na Mkuu wa utawala jeshini Gen.David Elazar kwa pamoja waliamua kuwaita wanajeshi wa anga wale wa akiba na wale wa vifaru wale wa akiba maana walijua hapo sasa vita haiepukiki.

 Kabla ya vita siku hiyo majeshi ya pande zote mbili yalikuwa na zana zilizokuwa zinakisiwa kuwa hivi:

 ISRAEL               

 Ndege za kivita 358 

 Vifaru 2100

   Meli za kivita 37

MAADUI ZAKE

Ndege za kivita 998

Vifaru 4350

Meli za kivita 137

 

 

 Ilipofika saa nane kamili mchana majeshi ya Msri na yale ya Syria yalianza kumimina makombora kuelekea katika sehemu zilizokuwa zinakaliwa na Israel,Misri na Syria zilichagua siku ya jumanosi maana ilikuwa ni sikukuu ya kiyahudi ya YOM KIPPUR waliona siku hiyo wayahudi wote huwa wanasherehekea hivyo ilikuwa upenyo mzuri sana kwao.

 Kwa upande wa Sinai majeshi ya Msri yaliweza kuvuka mfereji wa Suez kupitia sehem tano tofauti na kwa upande wa mizinga Misri iliweza kukipiga kituo cha wanaanga wa Israel waliokuwa Refidim katika jangwa la sinai na vikosi vingine vya mizinga vya Israel vilishasmbuliwa na mizinga ya Misri,na kufikia saa 11 jioni maelfu ya Wanajeshi wa misri walikuwa wamefika upande na kulikamata eneo lote la mashariki mwa mfereji wa Suez na wakati wa usiku vikosi vya vifaru vilivuka mfereji wa Suez hapo ndipo hali ya uwanja wa vita ilibadirika kabisa kwa Israel uwepo wa askari wa miguu wa Israel na mizinga yao hakukuweza kuyasimamisha majeshi ya Misri. Division ya 252 na Brigedi ya 14 ya kikosi cha vifaru viliadhirika vibaya sana asilimia kubwa ya vifaru vyao vilikuwa vimeangamizwa na silaha aina ya SAGGER ANT-TANK GUIDED MISSILES toka Misri.

 Jeshi la anga la Israel lilipoitwa ili kudhibiti majeshi ya Misri,Ndege hizo zilijikuta zinaangushwa na mizinga ya kuangushia ndege, Misri iliweza kuzitungua ndege za Israel kiasi cha kuzimalizia uwezo wa kushambulia na baada ya kujipanga vizuri na kujua namna ya kukwepa makombora ya kuangushia ndege aina ya SA-7 ndege za Israel ziliweza kuziangamiza helcopter zilizokuwa zimebeba Makamandoo wa misri na kuweza kuzitungua ndege 7 aina ya MIG kwenye uwanja wa mapambano. mapambano hayo yalifanyika kusini mwa mfereji wa Suez ndege hizo ziliangushwa na ndege za Israel aina ya PHANTOM.

 Kwa upande wa milima ya Golani majeshi ya Syria yaliweza kusonga mbele huku mizinga na vifaru pamoja na askari wa miguu waliweza kumiminia mizinga,risasi majeshi ya Israel kwa saa nzima mfululizo wakati huo Israel ilikuwa na Brigedi mbili za vifaru Division ya 36th ndiyo ilikuwa mstari wa mbele na Brigedi 188th nayo ilikuwa na jukumu la kulinda sehemu ya kusini ya mlima wa Golani na Brigedi ya 7th ilikuwa na jukumu la kulinda sehemu ya kaskazin mwa mlima Golan hivyo vifaru vya Israel havikuweza kuvishambulia vikosi vya Syria sababu havikuwa kwenye RANGE ya kuweza kushambuliwa.

 Mapigano ya vifaru yalianza tu siku hiyo baada ya jua kuzama majeshi ya Syria yaliweza kupenya ngome za Majeshi ya Israel kwa kuwa walikuwa wanatumia NIGHT-VISION viona usiku hivyo vilisaidia sana majeshi ya vifaru vya Syria vifaru vya Israel vilivyokuwa upande wa kaskazini havikuweza kufua dafu mbele ya vikosi vya Syria,vifaru vya Syria viliweza kushika sehemu ya kusini mwa mlima Golan na ilipofika asubuhi ya tarehe 07-10-1973 vifaru zaidi ya 600 vilikuwa vimeingia ndani ya ardhi ya Israel na vilikimbilia kwenda kulishika Daraja mhimu la nto Jordan na kambi ya kijeshi ya Nafar,Israel pia ilipoteza mlima wa HELMON ambao ulikuwa wa kimbinu strategic nao uliangukia mikononi mwa majeshi ya Syria hili lilikuwa pigo kubwa kwa majeshi ya Israel.

 Kwa upande wa majini majeshi ya Israel yaliweza kuziangamiza boat zilizokuwa zinabeba makombora za Syria na miji yote iliyokuwa inazunguka milima ya Golan wakazi wake waliondolewa na majeshi ya Israel.na baada ya siku 18 Majeshi ya Israel yaliweza kujijenga upya na kuchukua tena eneo lote la milima ya Golan na mlima Hermon

By Yericko Nyerere

CHADEMA imeng’ara kwenye Uchaguzi na Itashinda 2015

By

 Yericko Nyerere

Inawezekana kauli yangu isiwaingie watu masikioni mwao kabisa, lakini nitawaeleza japo kwa kifupi.

 Katika siasa kuna kitu kinaitwa siasa za jumla (general politics) na siasa za kijiografia (geography politics)

 General politics inahusu mambo yanayohusu siasa za kitaifa bila kuchagua chama au itikadi na hizi mara nyingi husimamiwa kwa katiba, kanuni na sheria za nchi, hapa inahusiana pia na daftari la wapiga kura na tume ya uchaguzi,

 Geography politics inahusu siasa za eneo husuka, kuna international gp, na domestic gp,

 Katika hayo Chadema ime win kwenye Gp-D kwa asilimia zaidi ya 90%, hili linatokana na chama kushiriki uchaguzi kwa miaka yote huku mambo muhimu yanayopaswa kufanywa kwenye General Politics yakiwa doro kabisa, mambo hayo ni kama tume kuwa huru, daftari la wapigakura kuboreshwa, na dola kuvuruga chagizi nyingi kwa maslahi ya ccm.

 Takwimu za chaguzi hizi zinatoa sura stahiki ya ubora wa domestic political ya Chadema,

 Mathalani uchaguzi huu Chadema ilikuwa ikitetea kata 3, za Nyaisura, Kiborloni na Mikol.. Kigoma.

 Tumepoteza Nyaisura, na Kigoma, na Tumeipoka ccm kata za Sombetini na Njombe.

 Thamani ya kata ilizoshinda chadema nikubwa kuliko ccm, kubeba kata ya njombe ni turufu kubwa, vivyo hivyo kata ya sombetini Arusha ambapo sasa rasmi ccm inakuwa chama cha upinzani Arusha, CCM hawajaongeza thamani yoyote ya kata,

 Kwa lugha nyingine nikuwa CHADEMA 0-0 CCM, lakini CHADEMA wananafasi ya golden goal kwakubeba kata ya Njombe ambayo kwanza inafuta propaganda za ccm yakuwa chadema ni chama cha ukanda, sasa tunashuhudia Chadema sio chama cha ukanda tena bali chama cha kitaifa na kila pembe ya jamhuri hii kipo.

 Izingatiwe kuwa oparesheni M4C Pamoja Daima haikuwa maalumu kwaajili ya uchaguzi huu bali sehemu ya ratiba ya chama katika kutoa elimu ya umma kudai/kuhimiza uboreshaji wa daftari la wapiga kura.

 Kuna wanaoamini kuwa Chadema kuwaadhibu wanachama wake waliovunja katiba ya Chama akina Zitto, Killa, Mwigamba eti ni “Mgogoro” uliochangia kwa 100% kutopata kata nyingi zaidi katika uchaguzi huu.

 Nikubaliane nao wale wafikirio hivyo lakini tupeane shule ya falsa ya siasa kidemorasia kwa ufupi ambayo ndio hutawala siasa za uwanda wa chama kinachojiandaa kushika dola.

 Niseme kuwa Chama cha siasa kilichokomaa na chenye wanachama wenye nguvu ya kitaifa kinapoamua kumuwajibisha mwanachama yeyote mwenye nguvu ya kitaifa aliyevunja katiba,itikadi,itifaki na falsafa ya chama hicho, kovu lake huwa halizibwi kwa miezi mitatu au sita tu, kisayansi itachukua hata mwaka kuirejesha nguvu ya chama katika mizani stahiki ya kisiasa.

 Hivyo Mwanachadema yeyote na mwanamageuzi ni lazima atambue kuwa uchaguzi wa Udiwani huu kwa kata 27 nchini, sio kipimo stahiki cha kufuta pengo la akina Zitto. Labda kwa mchambuzi wa siasa asiejua sayansi ya siasa tu na mwenye agenda ya kipropaganda ndie ataamini kufukuzwa akina Zitto ni chanzo cha kupata kushindwa kupata kura nyingi zaidi katika uchaguzi huu.

 Athari za kufukuzwa kwa Zitto na wenzie ndani ya chama zitapimwa baada ya miezi sita hadi mwaka mmoja kutoka sasa hii ikiwa na maana uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu ujao ndivyo vitakuwa vipimo vyake, kwa sasa yanayotokea yalitarajiwa kwa 100% na yalipita kwenye chekecho la kimkakati la chama na kisha yakaamuliwa iwe hivyo.

 Kosa kubwa kwa Chadema ni kosa la kimkakati na hili ni lazima lifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo,

 Kwanza ieleweke kuwa daftari la wapiga kura ndio rungu lililoibeba ccm, ni lazima liboreshwe ikiwa ni pamoja na uingizaji wawapiga kura wapya ambao utafiti unaonyesha ni kundi kubwa la vijana wenye umri kati ya miaka 18-26 ambao hawakuwa na sifa ya kupiga kura 2010. Lakini hata hawa waliojiandikisha yaani wenye kupiga kura sasa, idadi kubwa ya wapiga kura hao hawakupiga kura kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuuza shahada zao.

 Pili Tume ya Uchaguzi, hii ni lazima juhudi za msksudi zitumike kuitoa mikononi mwa chama tawala, ni hatari kuiacha iendelee kuwa wakala wa ccm badala yakuwa tume huru.

 Tatu Vyombo vya dola, hapa ndipo panahitaji mkakati mkuu wa kisiasa, jeshi la polisi ni lazima tukabiliane nalo na ieleweke vema kuwa ccm haitakoma kulitumia jeshi la polisi ama vyombo vya dola kwa ujumla mpaka siku inakata roho kabisa, hivyo njia mbadala ni muhimu sana tunapoelekea kushika dola hili la Tanzania mnamo octobar 25, 2015.

 Kwanza uundwe mkakati wa uhusiano mwema na vyombo vyote vya dola nchini, hili linaweza kuwa gumu kidogo na linaweza kuifanya serikali ianze kupata mafua ya msimu na kujikuta tunaingia kwenye mgogoro unaoweza kutumiwa na wakware wa akili wa ccm kama akina Mwigulu na kufikiria uhaini, jambo la muhimu ni kuziangalia sheria za nchi hasa zinazoratibu vyama vya siasa na mienendo yake,

 Mathalani kiongozi wa kisiasa kuzuru makao makuu ya Polisi Tanzania na kusikiliza changamoto zinazowakabilli, hili halina zuio kisheria, ilimradi haendi kugawa kadi za chama hapo,

 Ni lazima tuitazeme upya sheria inayosema mtumishi wa umma asijihusihe na siasa, hii ni nzuru lakini iboreshwe ili iwe na tafsiri ya maslahi kwa nchi na hatimae taifa kuzaa siasa za kisasa na za kimaendeleo.

 Wanamikakati warejee chini wawafanyie utafiti wa kisayansi viongozi wa majimbo, mikoa na kanda, nilazima tuwapime kwa nyuzi 360 kiutendaji kwakuwa hizi chaguzi ndogo za kata na serikali za mitaa zinatakiwa wao wasimamie na kuonyesha uwezo wao na sio hivyo tu bali lipo ndani ya uwezo wao kikatiba, Chama lazima sasa kijikite kwa nguvu zote kwenye msingi (chadema ni msingi).

 Ni lazima tufanye utafiti wa kimkakati usio na unafiki wala haya,

 Tukiyatekeleza haya yote, uchaguzi wa serikali za mitaa utaanza kutupa majibu ya mkakati huu na uchaguzi mkuu ujao tutashinda!

 Yote kwa yote Chadema haijapoteza uchaguzi huu bali imeng’ara, kimkakati ni ccm ndio imepoteza.

By Yericko Nyerere

Rwandan fugitives relocate to Tanzania

 

By Times Reporter  February 10, 2014      

 

Renegade army Captains, Charles Sande and Christopher Busigo, who are wanted by the Government of Rwanda on charges of subversion, fled to Tanzania from Uganda where they are coordinating their activities contrary to media reports that they were kidnapped, The New Times has learnt.

 A Ugandan newspaper, The Daily Monitor, reported on Saturday, February 8, that the two dissidents had disappeared.

  “We are aware of their plans. They are faking kidnap to evade  justice,” an official who preferred anonymity was quoted saying.

 “We understand that RNC is shifting camp from Uganda to Tanzania, and that the Kayumba Nyamwasa group is using some Ugandan journalists for propaganda purposes,” the source added.

 This newspaper has also learnt that Busigo now uses a Tanzanian line; +255712526565 to communicate with his superiors and other people.  Efforts to talk to Busigo were futile as by press time he had declined to answer our repeated calls.

 Police spokesperson, ACP Damas Gatare, also dismissed the kidnap claims, adding that the police will ensure that all the criminal suspects hiding in and outside the country are arrested and brought to book.  Gatare said there have been several cases where criminal suspects faked their kidnap in order to qualify for asylum in other countries.

 They include that of terror suspect, Lt. Joel Mutabazi, who is said to have staged his own shooting in Uganda and blamed the Rwandan government.

 Others include the vice-president of a faction of PS-Imberakuri, Alexis Bakunzibake, who recently led it into an alliance with the FDLR, a terror group whose members are largely responsible for the 1994 Genocide against the Tutsi. He too faked his kidnap in 2012, only to resurface some months later.

 And this month, former communications secretary of the Democratic Green Party of Rwanda, Omar Leo Oustazi, also returned to the country after a year in exile and dismissed reports that he had been kidnapped.

He went on to accuse his former boss, Frank Habineza, of being behind an alleged plot to have him killed and blame it on the government.

By Yericko Nyerere

Walikubali Mchakato wa Katiba Mpya wakubali na Matokeo yake.

By Mwanakijiji

 

Hawazi watu kuamka sasa na kulalamika kuwa ati Bunge la Katiba litakuwa limejaza CCM na kuwa Katiba Mpya itakuwa ni ya CCM! Haiwezekeni watu wapate ufunuo leo hii baada ya kutangazwa kwa majina ya wabunge wa  Bunge la Katiba ati sasa wametambua kuwa Kikwete anawachezea akili ati kwa vile wameona majina ya makada na wana CCM maarufu kama kina Kingunge Ngombare Mwiru, Shamim Khan, Paul Kimiti, Sixtus Mapunda, na Dr. Zainab Gama nikiwataja wachache tu.

Kuna watu wanataka tuamini kuwa makundi yaliyogawanywa katika matangazo ya majina hayo watajadiliana kimakundi kwenye Bunge la Katiba; kwamba wakulima watakaa kama wakulima na kujadiliana, wavuvi kama wavuvi, wanasiasa kama wanasiasa n.k. Ukweli ni kuwa sheria ya Katiba Mpya haijaweka utaratibu wa mijadala ya Makundi au kulazimisha kupiga kura kwa makundi. Hivyo watu wasifikirie kuwa ati kwenye Bunge la Katiba makundi yataulizwa na kupiga kura ili kutoa msimamo wao kama kundi. Sheria inatoa uhuru wa maoni na mijadala kwenye Bunge la Katiba na hivyo wabunge hawa hawafungwi na utii au umoja wa makundi yao!

Lakini jambo ambalo liko wazi – na nililionesha miaka miwili iliyopita – ni kuwa Bunge litajaa watu wenye maslahi na CCM hasa kwa vile ‘magenius’ wetu walikubali kuwa wabunge wote na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba. Kwa kutangazwa kwa majina haya watu wenye maslahi na CCM au ambao wamewahi kushika nafasi za uongozi ndani ya CCM wanaunda kundi kubwa zaidi (super majority) kwenye Bunge hili. Hili si jambo la bahati mbaya; siyo jambo ambalo linakuja tu hivi hivi na ukiangalia kwa karibu utaona kuwa ni jambo ambalo litahakikisha kuwa kile ambacho CCM wanataka wanakipata.

Sasa wapo waliokubali mchakato huu mbovu wa kuandika Katiba Mpya; walikubali kwa sababu waliamini – kwa makosa – kuwa utakuwa ni wa haki, wa wazi na ambao utawapa nguvu wananchi. Badala yake walikubali kumpa Rais wa JMT na Rais wa Zanzibar nguvu kubwa sana. Hivi kulikuwa na ubaya gani kwa taasisi kutaja wajumbe wake wa Katiba (wachaguliwe kwenye taasisi hizo kwa uhuru) badala ya kuachiwa Rais kuamua? Matokeo yake wapo baadhi ya wabunge hawa ambao wanamshukuru Rais leo hii kwa “kuwakumbuka” kwani wengine nyota zao za kisiasa zilishafifia!

Tulisema huu ni mchakato mbaya; na kama watu wanafikiri wameshaona ubaya wake wangoje mijadala ya Bunge hili itakavyoanza. Binafsi nitawakatalia wapinzani wakianza kulalamika kuwa wanaburuzwa au kuwa hawana imani na mchakato au na Rais! Hilo litakuwa ni kigeugeu kilichopitiliza! Yote ambayo yatatokea wapinzani wanajua na walishajulishwa na wakakaza shingo zao kuukumbatia mchakato huu haramu (ni haramu kwa sababu umevunja Katiba ya sasa).

Nitaendelea kuukataa na japo ninatamani sana kuona Tanzania inakuwa na Katiba Mpya nzuri na inayotokana na wananchi naamini kuwa mchakato huu hadi hivi sasa umewanyima Watanzania haki hiyo. Walioukumbatia toka mwanzo, wakatoa maoni na kutoa wajumbe na kukubali kuwa ni halali wasigeuke sasa; wametikisa dawa, sasa wainywe; wasiseme “chungu

By Yericko Nyerere

Kwanini Hayati Baba wa Taifa alitumia kura yake ya veto kumkataa Lowasa?

By Yericko Nyerere

 

“Kwanini Hayati Baba wa Taifa alitumia kura yake ya veto kumkataa Lowasa kwa sababu iliyoitwa na inayoaminika mpaka sasa kuwa “Lowassa ni MWIZI anautajiri mkubwa usio na ufafanuzi alioupata kwa mda mfupi tu akiwa mkurugenzi wa AICC?”

 Ikumbukwe nikuwa hoja hiyo ya Mwalimu Nyerere ilikuja baada ya Lowassa na wapambe wake kukodi ndege binafsi kutoka Arusha kwenda Dodoma kuhudhuria vikao vya uteuzi wa urais mwaka 1995, kitendo hiki kilimfedhehesha sana Mwalimu na wazalendo wengine na hata kufikia kuliondoa jina la fisadi huyu nguli wa Tanzania,

 Je leo utajiri wa Lowassa umekuwa halali?

 Mamlaka ya mapato Tanzania inaweza kututhibitishia uhalali wa kodi alipayo mtu huyu?

 Tangu afukuzwe uwaziri mkuu mwaka 2007 taarifa za kuaminika kutoka vyanzo muhimu nikuwa Lowasa alitenga 12bilioni kwaajili ya kujitakasa, ambapo mpaka leo hii ameshatumia 8bilioni, je pesa hii ameipata wapi? Imelipiwa kodi kiasi gani? Atairudishaje akiwa rais?

 Ili kuhuisha mjadala huu hebu niwaeleze jambo mhimu dhidi ya mtu huyu aitwae Edward Ngoyai Lowasa,

 Labda niwaelekeze watafiti watafute faili la EL la enzi za TANU pale Lumumba. Mzee Paul Sozigwa suala hili analifahamu fika.

 Ndiyo, Mwl. Nyerere alichukizwa na tabia ya Lowasa ya kujitajirisha kwa kuiba mali ya umma. Lowasa, licha ya tuhuma za wizi enzi akiwa AICC, kujimilikiaha majumba ya Masajili wa Majumba wakati akiwa waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo Mijini, Mwl. Nyerere alikuwa akifahamu wizi wa Lowasa tangu enzi za TANU. Kati ya mwaka 1974 na 1977 Lowasa aliiba pesa za TANU alizopewa kusamia ujenzi wa ofisi ya TANU Arusha. Badala ya kujenga ofisi ya TANU Lowasa alinunua kiwanja na kujenga nyumba yake binafsi. Jambo hilo lilipogundulika mwaka 1982, lilimkasirisha sana Mwl hivyo kuamuru afukuzwe kwenye chama. Ni marehemu Edward Moringe Sokoine ndiye alimwombea msamaha kwa Mwl. Nyerere abadilishiwe adhabu. Edward Lowasa alipewa adhabu mbadala; kuhudhuria kazini Ofisi Ndogo ya Chama Mtaa wa Lumumba kila siku bila kukosa, kuwa kazini masaa 8 bila kutoka lakini bila kupangiwa kazi yoyote hadi Chama kingeona ametubu na hatimaye apangiwe kazi nuingine. Lowasa alitumikia adhabu yake hadi Sokoine alipofariki.

 Hiyo ndio sababu kuu ya Mwl. Nyerere kumkatalia Lowasa kugombea urais.

 Kikwete, Mkuchika, Twaa Khalifan, Kinana, Bagenda na Msekwa wanajua ukweli wotekuhusiana na jambo hili. Ila maadamu kwa sasa hakuna tena maadili ya uongozi wa kisiasa nchini Tanzania, Lowasa anaweza kuachiwa awatawale wezi, wala rushwa na mediocre wa nchi hii.

 

“Kuna watu wasipokuelewa maneno na matendo yako, mshukuru Jah, wewe bado unafikra chanya, wakianza kukuelewa jichunguze ni wapi umeanguka maana umeanza kuwaza kama wao”

By Yericko Nyerere